WADAIWA KUNYWA DAWA ZA ARV BILA KUPIMA VIRUSI VYA UKIMWI

Mkurugenzi mkuu wa Tume ya Kupambana na Ukimwi Tanzania (Tacaids), Dk Leonard Maboko amesema Watanzania wengi wana mwamko wa kutumia dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi (ARV) kuliko kujua hali zao.

Dk Maboko alibainisha hayo jana wakati akizindua mpango mkakati wa miaka mitano wa taasisi ya kupambana na maambukizi ya virusi vya Ukimwi ya Agpahi.

“Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa asilimia 90 ya wajawazito wanajua hali zao kati yao, asilimia 98 wanatumia dawa za ARV. Hata hivyo, utafiti uliofanyika ilibainika kuna watu hawajui hali zao lakini walipopimwa damu zilionyesha tayari wanatumia ARV,” alisema.

Awali, mkurugenzi mtendaji wa Agpahi, Dk Sekela Mwakyusa alisema kupitia mpango huo wanatarajia kupanua wigo wa huduma ili kufika maeneo mengi zaidi na kuhakikisha maambukizi kwa watoto wanaozaliwa yanakoma.

Na Ephrahim Bahemu, Mwananchi 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527