MAGUFULI AWAPONGEZA UPINZANI, AWAPA AHADI YA KUENDELEZA USHIRIKIANO

Baada ya Mahakama Kuu ya Kikatiba ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kumtangaza Kiongozi wa upinzani, Bw. Felix Tshisekedi kuwa mshindi wa uchaguzi wa Urais, Rais John Magufuli amempongeza Rais huyo mteule na kumuahidi kuendeleza ushirikiano.

Rais Magufuli ametoa pongezi hizo leo Januari 20, ambapo mbali na kumpongeza Rais Mteule amewapongeza pia raia wa Kongo akiwataka kuduisha amani.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Magufuli ameandika, "Kufuatia hukumu ya Mahakama Kuu ya Katiba. Ninampongeza Felix Tshisekedi juu ya uchaguzi wake kama Rais wa DRC.

"Ninapongeza pia Wakongo wote, ninawasihi kudumisha amani . Ninaahidi kuendeleza uhusiano wetu wa kihistoria na wa kindugu" Rais Magufuli.

Katika uchaguzi huo uliofanyika Desemba 30 2018, Mgombea Martin Fayulu alidai kuwa ndiye mshindi wa kiti hicho cha Urais, amezitaka Jumuiya za kimataifa kutomtambua Tshisekedi, akidai kuwa yeye ndiye mshindi halali wa uchaguzi huo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527