Tanzia : ALIYEZAWADIWA MILIONI 100 NA JPM KWA KUGUNDUA MADINI YA TANZANITE AFARIKI DUNIA


 
Mvumbuzi wa madini ya Tanzanite, Jummane Ngoma enzi za uhai wake

Aprili 6 ,2018, Rais John Magufuli akiwa na mzee Jumanne Ngoma wakati akizindua ukuta wa mgodi wa Tanzanite, Mirerani mkoani Manyara ambapo Rais Magufuli alimzawadia Sh100 milioni kama shukrani kwa mchango wake kwa kugundua madini ya Tanzanite.

Mvumbuzi wa madini ya Tanzanite, Jummane Ngoma amefariki dunia leo Jumatano Januari 30, 2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mtoto wa marehemu, Hassan Ngoma,akizungumza na Mwananchi  amesema, “Ni kweli Mzee amefariki leo jioni hii hapa Muhimbili,” amesema Ngoma.

Hassan amesema kinachofanyika kwa sasa ni kuuhifadhi mwili wa baba yake kisha baadaye watatoa taarifa rasmi ikiwamo utaratibu wa msiba utakuwa wapi na mazishi yatafanyika wapi baada ya kikao cha familia.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527