KUZIONA SIMBA NA JS SOUARA LAKI MOJA


Klabu ya soka ya Simba imetangaza viingilio vya mchezo wao wa klabu bingwa Afrika Jumamosi hii dhidi ya JS Souara kwenye uwanja wa taifa Dar es salaam.

Simba kupitia kwa msemaji wake Haji Manara imesema kiingilio cha chini ni shilingi 5,000 huku cha juu kikiwa ni laki moja.

''Viingilio vya mchezo mzunguko ni 5,000 huku VIP B ikiwa ni 10,000 lakini tutakuwa na tiketi za Platinums ambayo ni 100,000 itajumuisha kuchukuliwa na 'Luxury bus' kutoka Serena Hotel na kusindikizwa na polisi, jezi mpya ya Simba, 'Bites na soft drinks' muda wote utakaokuwa uwanjani pamoja na kurejeshwa Serena'', - Manara.

''Tunawasihi sana wanasimba na washabiki wote tujae kama kawaida yetu Jumamosi, na tuje kuhanikiza, tuje tukijua ujaji wetu ndio silaha yetu'', ameongeza Manara.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527