RAPPER OCTOPIZZO AINGIA KWENYE TUHUMA NZITO ZA MAUAJI YA MWANAFUNZI

Msanii wa Hip Hop nchini Kenya, Octopizzo Jana Jumapili 20, 2019 ametuhumiwa kwa mauaji ya mwanafunzi wa chuo kikuu cha 
Strathmore kilichopo jijini Nairobi.Octopizzo

Familia ya mwanafunzi huyo, imesema kuwa kijana wao alijeruhiwa katika nyumba ya Octopizzo kabla ya kujirusha kwenye ghorofa siku ya Jumamosi iliyopita.

Mwanafunzi huyo aitwaye, Kenneth Abom (19) inaelezwa kuwa kabla ya kuaga dunia alishambuliwa kwa panga na watu wasiojulikana na baadae alijirusha kutoka kwenye ghorofa baada ya kufanyiwa matibabu.

Tayari rapper Octopizzo, amekanusha taarifa hizo, ambapo amekiambia kituo cha NTV Kenya kuwa kijana huyo alipitia nyumbani kwake akiwa tayari amejeruhiwa na vitu vyenye ncha kali kichwani.

Octopizzo amesema Alhamisi iliyopita kijana huyo, alikatiza kwenye nyumba yake akiwa na majeraha hayo na kumshauri aende hospitali.

Baadae Octopizzo akaja kusikia, kijana huyo amejirusha kutoka ghorofani baada ya kupatiwa matibabu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527