RATIBA YA LIGI KUU BARA YAPANGULIWA


Ratiba ya ligi kuu soka Tanzania bara, imepanguliwa kwa mchezo mmoja kusogezwa mbele.

Mchezo huo ni namba 220 ambao ulikuwa unazikutanisha timu za KMC ya Kinondoni dhidi ya Coastal Union ya Tanga.

Awali ulipangwa kuchezwa Jumatano Januari 16, 2019 lakini sasa utapigwa Alhamis Januari 16, 2019 kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Ligi kuu hiyo ipo kwenye raundi ya pili mechi za 20 kwa baadhi ya timu huku Simba ndio ikiwa timu yenye viporo vingi zaidi ambapo imecheza mechi 14 pekee.

Msimamo unaongozwa na Yanga wenye alama 50 katika mechi 18 huku Tanzania Prison ikiwa na alama 12 katika nafasi ya 20 ikiwa imecheza mechi 19.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527