CCM YAGOMA KURUDI KWENYE CHAMA KIMOJA TANZANIA


Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema wanaodhani kuwa chama hicho kinataka mabadiliko ya sheria ya vyama vya siasa ili nchi irudi kwenye mfumo wa chama kimoja wanakosea.

Akizungumza na wanachama wa CCM mkoani Dodoma leo katika mkutano wa kukusanya maoni kuhusu Muswada wa sheria ya Vyama vya siasa, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt..Bashiru Ali amesema mfumo wa vyama vingi umeiimarisha CCM.

"Sheria hii si ya kwanza kutungwa na haitakuwa sheria ya mwisho...Ukiendesha siasa kwa urasimu hutatenda haki", amesema.

Amebainisha kuwa wanatetea muswada huo kwasababu umeongeza uhakika wa utawala na kulinda misingi ya utaifa.

Aidha Dkt. Bashiru ameongeza kwamba, "Mimi natamani sana kwenye sheria hii hata koma(alama ya nukta) isiondolewe lakini mnaweza kutoa maoni yenu ya kuboresha ambayo hayaondoi maudhui", ameongeza Dkt. Bashiru.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. 

Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527