SIMBA YAVUNJA MWIKO WA MIAKA 15..YAIRARUA NKANA RED DEVILS BILA HURUMA



Wachezaji wa Simba na Nkana wakati wa mchezo.

Klabu ya soka ya Simba imefanikiwa kutinga hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika ikiwa ni mara ya kwanza kwa timu ya Tanzania kufika hatua hiyo tangu walipofanya hivyo Simba mwaka 2003.

Simba imetinga hatua hiyo baada ya kushinda mabao 3-1 dhidi ya Nkana Red Devils ya Zambia kwenye mchezo wa marudiano uliomalizika jioni hii kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaa.

Mabao ya Simba yamefungwa na Jonas Mkude akisawazisha bao la Bwalya kabla ya Meddie Kagere kufunga bao la pili sekunde chache kabla ya mchezo kwenda mapumziko.

Simba sasa inaingia hatua ya makundi ikiwa na kumbukumbu ya kupangwa Kundi A miaka 15 iliyopita. Kundi hilo lilikuwa na timu za Enyimba ya Nigeria, Ismailia ya Misri na ASEC Mimosas ya Ivory Coast.

Kwa upande wa wachezaji wa Simba sasa Clatous Chama, amefikisha mabao 4 kwenye mechi 4 za hatua ya huku pia akiwa ametengeneza mabao takribani 4 kati ya 12 waliyofunga katika mechi 4.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527