MTIBWA SUGAR KUJENGA UWANJA MKUBWA WA SOKA

Klabu ya soka ya Mtibwa Sugar imetangaza nia yake ya kujenga uwanja wa kisasa na mkubwa wa soka, ambao utakuwa na uwezo wa kubeba mashabiki wengi zaidi.


Hayo yamezungumzwa na Mkurugenzi wa klabu hiyo, Jamal Bayser ambapo amesema kuwa wameamua kuwafuata mashabiki wao na wapenda soka kwa kuwajengea uwanja karibu na makazi yao.

"Dhumuni letu hasa ziadi ni kujenga uwanja ambao utakuwa karibu zaidi kule na wananchi, kule kuna maeneo wanaita Mabawa, ni eneo ambalo wananchi wengi wa Madizini pale wanaweza kutembea kidogo kuliko kule Manungu ambako ni ni mbali kwao," amesema Mkurugenzi huyo wa Mtibwa.

Mtibwa Sugar inajiandaa kwaajili ya mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya KCCA ya Uganda utakaopigwa wikiendi hii Jijini Dar es salaam.

Katika mchezo wa kwanza uliofayika mjini Kampala Uganda wikiendi iliyopita, Mtibwa Sugar ilifungwa kwa mabao 3-0, ambapo katika mchezo wa marudiano inahitaji ushindi wa mabao 4-0 ili iweze kusonga mbele katika hatua inayofuata.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527