KIVULINI, I4ID WAWASILISHA MAPENDEKEZO YA ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO KWA WAJASIRIAMALI ILEMELA


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza, John Wanga akizungumza kwenye kwenye kikao maalum/ cha dharura cha Baraza la Madiwani kilicholenga kujadili mapendekezo ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo,  leo Disemba 22, 2018.
Mhadhiri kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Dkt. Nasibu Mramba akiwasilisha mada kwenye kikao maalum/ cha dharura cha Baraza la Madiwani kilicholenga kujadili mapendekezo ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo.
Mhadhiri kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Dkt. Nasibu Mramba akiwasilisha mada kwenye kikao maalum/ cha dharura cha Baraza la Madiwani kilicholenga kujadili mapendekezo ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo.
Mratibu wa Sekta isiyo rasmi Manispaa ya Ilemela, Raphael Mphuru (kulia), akiwasilisha mapendekezo ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Shiriki la kutetea haki za wasichana na wanawake KIVULINI, Yassin Ally.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, Renatus Mulunga (katikati), Kaimu Naibu Meya Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, Alfred Wambura (kushoto) pamoja na Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, Shukrani Kyando (kulia), wakifuatilia mada wakati wa kikao maalum/ cha dharura cha Baraza la Madiwani kilicholenga kujadili mapendekezo ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo.

Shirika la kutetea haki za wasichana na wanawake KIVULINI kwa kushirikiana na taasisi ya I4ID limewasilisha mapendekezo ya zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza.

Mapendekezo hayo yamewasilishwa leo Disemba 22,2018 kwenye kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Ilemela, kabla ya zoezi hilo la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo kuzinduliwa rasmi Alhamisi Disemba 27,2018.

Hatua hiyo imejiri baada ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kuzishirikisha taasisi hizo kama mdau wa maendeleo katika Halmashauri hiyo lengo likiwa ni kuhakikisha zoezi hilo linakuwa na mafanikio makubwa hususani vitambulisho hivyo kuwafikia walengwa.

Miongoni mwa mapendekezo yaliyowasilishwa ni pamoja na uundaji wa Kamati Maalum ya kusimamia zoezi la ugawaji vitambulisho hivyo ambayo inajumuisha Watendaji wa Kata, Watendaji wa Mtaa, Polisi Kata, Maafisa Maendeleo, Maafisa Biashara, Viongozi wa Wajasiriamali wadogo (Mwenyekiti na Katibu), Mwakilishi wa Wajasiriamali Wanawake pamoja na Mwakilishi wa Wajasiriamali Vijana.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga pamoja na Mkurugenzi wa KIVULINI, Yassin Ally kwa pamoja wamesema lengo ni kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa na mafanikio makubwa na Halmashauri hiyo inakuwa ya mfano nchini kwa kutekeleza vyema zoezi la ugawaji vitambulisho vya wajasiriamali wadogo.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527