JINSI WATUMIAJI WA DAWA ZA NYWELE WANAVYOWEZA KUPATA VIPARA


WATUMIAJI dawa za kisasa za kulainisha nywele wapo katika uwezekano mkubwa wa kupata matatizo ya ngozi na kunyonyoka nywele siku za usoni (kuwa vipara).

Hayo yalielezwa Dar es Salaam jana na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani, Grace Shayo wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), alipozungumza na MTANZANIA katika mahojiano maalumu.

Alisema hali hiyo inaweza kuwapata watumiaji kwani baadhi ya kemikali zilizochanganywa kutengeneza dawa hizo zinapotumika huenda kuathiri afya ya ngozi.

“Ni kweli matumizi ya dawa za nywele yanaweza kusababisha mtumiaji kuishia kupata matatizo ya ngozi, kuna wakati mtu akipakwa dawa hizi ngozi yake huungua.

“Kutokana na kule kuungua, kama ngozi ya kichwa itapona na kuacha kovu, basi sehemu hiyo yenye kovu inaweza isiote nywele tena kama ilivyokuwa hapo awali katika maisha yake,” alisema.

Na Veronica Romwald-Mtanzania

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527