CCM Yasema Mwisho wa Kuwapokea Wanaohamia Toka Vyama Vingine ni Novemba 15....Haya Hapa Maamuzi ya Kamati Kuu

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimewapitisha makada wake wanne kuwania nafasi ya ubunge katika maeneo yao kufuatia kikao cha kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kukutana leo jijini Dar es salaam.


CCM imewapitisha waliokuwa wabunge wa maeneo hayo kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), waliotangaza kujiunga na chama hicho kwa sababu mbalimbali ikiwemo kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli.

Wabunge hao waliopitishwa ni Pauline Gekui wa jimbo la Babati, James Milya jimbo la Simanjiro, Joseph Mkundi Jimbo la Ukerewe, na Marwa Ryoba ambaye atawania nafasi ya ubunge jimbo la Serengeti.

Aidha Chama hicho kimetaja tarehe 15 novemba kuwa ndio tarehe ya mwisho kwa Chama hicho kuwapokea maombi ya wenye nia ya kujiunga na Chama hicho na kupewa dhamana ya uwakilishi kupitia tiketi ya CCM kwa wabunge na madiwani kutoka vyama vingine.

Aidha taarifa hiyo imesema baada ya tarehe hiyo hakuna kiongozi yeyote atakayepewa nafasi ya kugombea uwakilishi wa Chama hicho katika uchaguzi wa marudio badala yake watakuwa wanachama wa kawaida.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527