MAKAMU MKUU WA CHUO KIKUU ARDHI AZINDUA MAFUNZO YA VYUO VIKUU 12 VYA AFRIKA KUHUSU MBINU NA NAMNA YA KUTATHMINI ATHARI ZITOKANAZO NA MAAFA


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) Profesa Evaristo Liwa akiongea machache wakati wa ufunguzi wa semina ya wiki mbili ya washiriki wa kozi ya kimataifa kuhusu maafa inayondeshwa na Chuo Kikuu Ardhi ikiwalenga wanafunzi wa shahada za juu na watendaji wa taasisi za kiserikali, binafsi na mashirika ya kimataifa jijini Dar es Salaam. Washiriki wanatoka nchi 12 za Afrika na Taasisi ya World Food Programme (WFP) Wakufunzi wanatoka Vyuo Vikuu vya Afrika vinavyounda mwamvuli wa Periperi U, UNDP na WHO Kozi hiyo imefadhiliwa na UNDP, USAID, WHO na WFP. Kushoto ni Kaimu Naibu Mkuu Chuo Mipango, Fedha na Utawala, Profesa Robert Kiunsi. (Imeandaliwa na Robert Okanda) 
Sehemu ya washiriki wa semina ya kozi ya mafunzo ya mbinu za namna ya kutathmini athari zitokanazo na maafa wakifuatilia matukio wakati wa ufunguzi wa semina hiyo Dar es Salaam leo Septemba 10 2018. 

Mkurugenzi wa Utafiti wa Majanga na Mratibu Mratibu wa Mradi wa Periperi kutoka Chuo Kikuu cha Stellenbosch Dk Ailsa Holloway akiongea wakati wa ufunguzi wa semina ya kozi hiyo. 
Sehemu ya washiriki wa semina ya kozi ya mafunzo ya mbinu za namna ya kutathmini athari zitokanazo na maafa wakifuatilia matukio wakati wa ufunguzi wa semina hiyo Dar es Salaam leo Septemba 10 2018. 
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (Taaluma), Profesa Gabriel Kassenga (katikati) akibadilishana mawazo na Makamu Mkuu wa ARU, Profesa Evaristo Liwa (kulia) baada ya ufunguzi wa semina hiyo Dar es Salaam leo Septemba 10 2018. Kushoto ni Kaimu Naibu Mkuu Chuo Mipango, Fedha na Utawala, Profesa Robert Kiunsi. 

Mgeni rasmi Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) Profesa Evaristo Liwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa semina ya kozi ya mafunzo ya mbinu za namna ya kutathmini athari zitokanazo na maafa Dar es Salaam leo Septemba 10 2018. 

Sehemu ya wanahabari wakifanya mahojiano na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) Profesa Evaristo Liwa. Kushoto ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (Taaluma), Profesa Gabriel Kassenga.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527