NUSU FAINALI YA KWANZA KOMBE LA DUNIA LEO...UFARANSA,UBELGIJI KUUMANA


Nusu ya fainali ya kwanza ya michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi inaanza leo kwa mchezo mmoja kupigwa katika Uwanja wa Saint Petersburg baina ya Ufaransa na Ubelgiji.


Mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu na asilimia kubwa ya wadau wengi soka duniani itaanza majira ya saa 3 kamili usiku wa leo.


Mpaka sasa Ufaransa waliowahi kutinga hatua ya fainali mwaka 2006 dhidi ya Italia, wamepewa asilimia kubwa ya ushindi kuliko wapinzani wao Ubelgiji.


Ufaransa na Ubelgiji zimekutana mara 73 katika mashindano yote huku Ubelgiji wakishinda mara 30 na Ufaransa wakishinda mara 24 pamoja na kwenda sare mechi 19, leo watakuwa wanakutana mara ya 74.


Vilevile timu hizi kukutana mara ya mwisho katika michuano hii ilikuwa ni mwaka 1986 ambapo Ufaransa iliweza kushinda mabao 4-2 katika hatua ya kusaka mshindi wa tatu.


Na katika mchezo wa mwisho ambao ulikuwa wa kirafiki, Ubelgiji waliibuka na ushindi wa mabao 4-3 jijini Paris, mwaka 2015.


Kesho kutakuwa na mchezo mwingine wa pili ambapo England iliyokuwa haipewi nafasi kubwa kufanya vizuri, itakuwa inacheza na Croatia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527