Breaking : AJALI YAUA TENA MBEYA...MAGARI MATATU YAGONGANA



Watu watano wanadaiwa kufariki dunia  katika ajali iliyohusisha lori pamoja na gari dogo aina ya Noah eneo la mteremko wa mlima Igawilo nje kidogo ya jiji la Mbeya usiku wa Alhamis Julai 5,2018 .

Ajali hiyo iliyohusisha magari matatu imetokea kwenye mteremko wa mlima Igawilo na kwa mujibu wa mashuhuda gari lenye kontena ililiangukia gari aina ya Noah iliyokuwa na abiria na inasadikiwa watu watano wamepoteza maisha.

Ajali hii imetokea ikiwa ni muda mfupi tu baada ya Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola kutembelea Mbeya na kutangaza kuvunja Baraza la Taifa la Usalama Barabarani pamoja na Kamati zake zote za Mikoa na Wilaya



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527