MWANZA KUADHIMISHA SIKU YA HEDHI DUNIANI MEI 28, 2018



Meneja Mradi (Elimu Bora) shirika la TAYONEHO,James Edward

Tanzania kesho inaungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha “Siku ya Hedhi Duniani” ambapo kwa mkoa wa Mwanza maadhimisho yatafanyika katika uwanja wa Furahisha Manispaa ya Ilemela.

Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka Mei 28 ambapo hii ni mara ya pili Tanzania kuadhimisha maadhimisho hayo tangu kuasisiwa na Umoja wa Mataifa UN mwaka 2014. Kitaifa mwaka jana yalifanyika mkoani Dodoma.

Kama ilivyokuwa mwaka jana, shirika la Tanzania Youth With New Hope in Life Organization (TAYONEHO) la Jijini Mwanza kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la Plan International limeandaa maadhimisho ya mwaka huu kama anavyoeleza zaidi James Edward ambaye ni Afisa Mradi (Elimu Bora) TAYONEHO.
Na BMG

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527