SERIKALI YAKIRI KUJICHANGANYA KIGEZO CHA UMRI WA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO NA SITA

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Avemaria Semakafu amefunguka na kuweka wazi utata ulioibuka kuhusu kigezo cha umri wa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na sita na kusema taarifa ambayo inasambaa imekuwa na makosa.

Semakafu amesema kuwa yametokea makosa ya kiuandishi ila kujiunga na masomo ya kidato cha tano na sita ni miaka 25 na siyo miaka 20 kama ambavyo inasomekana katika taarifa aliyotolewa jana

"Kumetokea makosa ya kiandishi, miaka ni 25 ya kujiunga sekondari na sio 20 kama ambavyo inasomeka kwenye ile karatasi" alisema Semakafu 


Kufuatia makosa hayo serikali imetoa waraka mpya kurekebisha ule wa mwanzo, na kipengele cha miaka 20 wameweka 25.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527