RAIS MAGUFULI AMTEUA JANETH MASABURI KUWA MBUNGE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bi. Janeth Masaburi kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Rais Magufuli amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayompa mamlaka ya kuteua wabunge 10 watakaokuwa miongoni mwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Bi. Janeth Masaburi ataapishwa kulingana na taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post