TUME YA UCHAGUZI YA KENYA YATANGAZA TAREHE YA UCHAGUZI WA RAIS

Tume huru ya uchaguzi nchini Kenya IEBC imetangaza rasmi tarehe ya uchaguzi wa urais, ambao utakuwa wa marudio baada ya Mahakama kuufuta wa awali

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na tume hiyo kwa vyombo vya habari kupitia mitandao ya kijamii ukiwemo wa twitter, IEBC imesema Oktoba 17 ndiyo tarehe rasmi ya kufanyika uchaguzi huo.

"Uchaguzi mpya utafanyika Oktoba 17 mwaka 2017, kufuatia uamuzi wa Mahakama ya Juu wa kufuta uchaguzi wa urais uliofanyika Agosti 8, 2017, hakutakuwa na wagombea wapya, wagombea ni Raila Odinga na mwenzake Kalonzo Musyoka, pia Uhuru Kenyatta na mwenzake William Ruto", iliandika taarifa hiyo.

Uchaguzi huo ulitakiwa kufanyika ndani ya siku 60 tangu uamuzi wa Mahakama ya juu wa kuufuta ule wa awali kutolewa, Septemba 1 mwaka huu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post