RAIS MAGUFULI AVUNJA MAMLAKA YA UENDELEZAJI WA MJI WA KIGAMBONI

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli amevunja Mamlaka ya uendelezaji wa Mji wa Kigamboni (KDA) kuanzia leo Septemba 13, 2017.


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Hashim Mgandilwa amethibitisha hilo na kusema kuwa Rais Magufuli ni msikivu kwani amesikia kilio cha watu wa Kigamboni na kuamua kuivunja mamlaka hiyo ya Uendelezaji wa Mji wa Kigamboni (KDA).


"Usikivu ni sehemu ya utatuzi hatimaye Rais wa Jamhuli ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli aridhia uvunjwaji wa Mamlaka ya uendelezaji wa mji wa Kigamboni (KDA). Akizungumza Waziri wa Ardhi Mhe. Lukuvi leo katika ukumbi wa chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere amesema "Mhe. Rais ameniagiza niwaalifu kuwa leo amevunja rasmi KDA, Ahsante Mhe. Rais kwa kutusikiliza" alisema Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mgandilwa


Mwezi Juni, mwaka huu Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile aliiomba serikali kukabidhi majukumu yote, yaliyokuwa yakifanywa na KDA kwa Halmashauri ya Manispaa hiyo ili kuyatekeleza na kuendeleza mji mpya wa Kigamboni.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527