MTOTO MWENYE UALBINO AUAWA KWA KUNYOFOLEWA UBONGO

Mvulana wa umri wa miaka 17 ambaye ana ulemavu wa ngozi amepatikana akiwa ameuawa na ubongo wake kutolewa nchini Msumbiji.

Mkazi wa eneo la Tete, magharibi mwa Msumbiji, ambaye hakutaka jina lake litajwe, amesema wazazi wa mvulana huyo walianza kumtafuta alipokosa kurejea nyumbani.

Mwili wake ulipatikana ukiwa hauna mikono na miguu.

Aidha, kichwa chake kilikuwa kimepasuliwa na ubongo wake kutolewa.

Msemaji wa polisi wa mkoa wa Tete Lurdes Ferreira amesema polisi wataanzisha uchunguzi eneo ambalo uhalifu huo ulitokea.

Kisa hicho ndicho cha karibuni zaidi dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi ambao mara kwa mara hushambulia kwa sababu ya viungo vyao ambavyo hudaiwa kutumiwa katika ushirikina.
Chanzo-BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527