![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifHEMM8FwUWBbDHEL31r08dB1ObPX-qfciKCHQ6v7PTr3lpTAoBOQzTOQFT-_A5YIa85e0qT9Zb2r_bNSNd3Vl7847n4QRjVv9RTci0MgLtC0BjoepMOkCVsb-eCsqGNQmOAKG9LUvVtg/s640/wabunge%252Bcuf.jpg)
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam leo August 4, 2017 imetupilia mbali pingamizi la Wabunge 8 wa Viti Maalumu waliofutwa uanachama na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Prof. Ibrahim Lipumba ya kutaka wabunge wateule 8 wasiapishwe na Bunge.
Uamuzi huo, umetolewa na Jaji Lugano Mwandambo ambaye amesema ametupilia mbali pingamizi hilo la zuio la kuapishwa kwa Wabunge hao 8 na kwa mantiki hiyo, Wabunge wapya walioteuliwa kuziba nafasi zao wanaweza kuapishwa.