SHABIKI MTOTO MATATA WA SOKA BRADLEY LOWERY AMEFARIKI DUNIA

Kama ni shabiki wa soka la England najua jina la Bradley Lowery sio geni katika masikio yako kutokana na umaarufu wa mtoto aliyekuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kansa kupenda sana kuishabikia Sunderland.
Bradley ambaye alikuwa ana mapenzi na Sunderland amefariki leo baada ya kusumbuliwa na kansa kwa muda mrefu, Bradley alikuwa akimpenda sana mshambuliaji wa zamani wa Sunderland ambaye amejiunga na AFC Bournemouth Jermain Defoe.

Shabiki huyo mtoto wa Sunderland aligundulika kuwa ana kansa akiwa na umri wa miezi 18 lakini amefariki leo akiwa na umri wa miaka 6, taarifa za kifo cha Bradley kimetolewa kupitia mitandao ya kijamii na wazazi wake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post