RAIS WA TFF JAMAL MALINZI NA KATIBU WAKE WARUDISHWA RUMANDE HADI AUGUST 11


Kesi inayomkabili Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, TFF, Jamali Malinzi na wenzake imeendelea leo July 31, 2017 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusogezwa tena mbele hadi August 11, 2017 kwa sababu upelelezi haujakamilika.


Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi haujakamilika ambapo hata hivyo, Mawakili wa washtakiwa, James Bwana na Abraham Senguji hawakuwa na pingamizi na suala la upelelezi.


Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi August 11, 2017.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527