HII HAPA TAARIFA YA WIZARA YA FEDHA,IMEOMBA BUNGE LIIDHINISHE SH 11.75 TRILIONI

Wizara ya Fedha na Mipango imeliomba Bunge iliidhinishie Sh11.757trilioni ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa mwaka wa fedha 2017/2018, kwa mafungu yote tisa yaliyo chini ya Wizara hiyo.
 
Maombi hayo yametolewa jana na Waziri wa Fedha na Mipango Philip Mpango, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizaya hiyo, Bungeni Mjini Dodoma.
 
Dk Mpango alisema kuwa kati ya fedha hizo, Sh10.328trilioni  ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh1.429trilioni  ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
 
Alifafanua kuwa matumizi ya kawaida yanajumuisha Sh87.996bilioni kwa ajili ya mishahara, Sh778.6bilini kwa ajili ya matumizi mengineyo (OC) na Sh9.4trilioni ni kwa ajili ya kulipa Deni la Taifa na Huduma nyingine.
 
Pia katika fedha za matumizi ya maendeleo, Sh1.382trilioni  ni fedha za ndani na Sh46.1bilioni ni fedha za nje.

==>Isome hapa hotuba ya bajeti ya Wizara  Hiyo  hapo chini


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527