Video:JINSI MWANAMKE MJANE ALIVYOZUA TAFRANI MBELE YA RAIS MAGUFULI

Jana katika uzinduzi wa mwaka mpya wa kimahakama jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Rais Dkt John Pombe Magufuli. Rais Magufuli alizungumza mambo mengi ambapo alipongeza Mahakama kwa kufanya kazi nzuri ya kutatua kesi mbalimbali kwa mwaka mmoja uliopita.



Aidha, Rais Dkt Magufuli alielezea baadhi ya changamoto zinazokabili muhimili wa mahakama ambapo alisema kuwa tatizo la rushwa limekuwa likisababisha kukosekana kwa haki kwa atu wanyonge huku kesi nyingine zikicheleweshwa kwa makusudi. Rais Dkt Magufuli amewataka watumishi wa mahakama kuhakikisha wanatoa huduma bila upendeleo.


Baada ya kuzungumza huko, tafrani kubwa ilizuka baada ya mama mmoja kunyanyuka akiwa na kitambaa kilichoandikwa jumbe mbalimbali kuelekea kwa Rais akionyesha kudhulumiwa haki yake huku mahakama na polisi wakihusika.


Hapa chini ni video ya tukio hilo;

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post