MSANII TID AWAOMBA RADHI WATANZANIA KWA TABIA YAKE KWA KUTUMIA DAWA KULEVYA

Msanii TID amefunguka na kuwaomba radhi Watanzania kutokana na tabia yake ya kutumia dawa za kulevya kwani anaamini kuwa akiendelea kutumia dawa hizo hatakuwa mfano bora hata kwa mtoto wake.

TID anasema anaamini kutokana na matumizi ya dawa hizo huenda akawa amewakwaza watu au kufanya mambo ambayo si mema katika jamii hivyo anaomba kusamehewa kwani alikuwa akifanya kwa nguvu ya dawa za kulevya na si yeye.

"Nimekuwa muathirika na matumizi ya dawa za kulevya, leo sipo hapa kusema kwanini nimeingia huku, nimekuja hapa kama kijana niliyepotea njia. Kutoka moyoni, nimekuja kukiri kuwa nimeikosea sana familia yangu, mama yangu, ndugu jamaa na marafiki hivyo nimekuja kuwaomba msamaha wote niliowakwaza under influence ya dawa za kulevya" alisema TID

Mbali na hilo TID anasema ameamua kuungana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaan Mhe. Paul Makonda katika vita dhidi ya madawa ya kulevya na kusema hata kama watu wanaweza kumuona mnafiki si mbaya maana yeye, ameamua kutoka katika matumizi ya dawa za kulevya.

"Nimesimama hapa kama kijana shupavu, mpambanaji, mnyama. Vita hii inabidi uwe mnyama kama Paul Makonda ili uweze kushinda, hakuna anayejua nimepitia mangapi mpaka nimefika hapa, natangaza rasmi kujiunga kwenye vita hii" alisema TID

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post