KUHUSU MWANZILISHI WA TOVUTI YA JAMIIFORUMS KUKAMATWA NA POLISI

Mwanzilishi wa tovuti ya JamiiForums, Maxence Melo amekamatwa na Polisi jijini Dar es Salaam kwa kukataa kutoa taarifa za watumiaji wa mtandao huo.

Taarifa kutoka kwenye tovuti hiyo zinaeleza kuwa Melo amenyimwa dhamana hivyo atalazimika kukaa rumande mpaka kesho atakapofikishwa mahakamani.

Jeshi la Polisi linadai kuwa Melo amekataa kuonyesha ushirikiano kwa Jeshi hilo ambapo walikuwa wakihitaji majina ya baadhi ya watumiaji wa mtandao huo.

JamiiForums wameeleza kuwa kiongozi huyo (Maxence) alikataa kutoa taarifa hizo kwa kile alichoeleza kuwa kufanya hivyo ni uvunjwaji wa Sheria na Haki za wananchi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post