ALIYEKUFA MUDA MFUPI BAADA YA KUBATIZWA KIKRISTO AZIKWA KIISLAM

Kijana Issa Juma aliyeripotiwa kufariki dunia Jumapili iliyopita, muda mfupi baada ya kubadili dini na kubatizwa katika mto mmoja kwa imani ya Kikristo akijiunga na kanisa la Efatha kwa jina la Paulo, amezikwa kwa imani ya Kiislam.


Uamuzi huo umefikiwa baada ya kuwepo mvutano kati ya Kanisa la Efatha na viongozi wa dini ya Kiislam wakitaka kijana huyo azikwe kwa imani yao, lakini mwisho kauli ya wazazi wa marehemu ilikuwa na nguvu zaidi na hivyo kuzikwa kwa imani ya Kiislam.


Akizungumzia uamuzi huo, mama mdogo wa marehemu ambaye jina lake halikupatikana alizungumza kwa niaba ya mama mzazi, Rehema Juma alithibitisha kuwa walimzika ndugu yao Jumanne wiki hii kwa imani ya Kiislam.


Kifo cha kijana huyo kiliibua sintofahamu ikiwa ni saa chache baada ya kuzaliwa kwa mara pili kwa imani ya Kikristo na haikufahamika mara moja chanzo chake kama alikuwa na ugonjwa ama ni masuala ya kiimani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post