WAMAREKANI WAANDAMANA KUPINGA USHINDI WA TRUMP

Kufuatia kutangazwa kwa Donald Trump kuwa rais mteule wa Marekani, wananchi wa Marekani wameandamana katika miji saba kupinga ushindi huo wa Trump.


Waandamanaji hao wamekusanyika nje ya mnara maarufu wa Trump ‘ Trump Tower’ mjini New York wakipaza sauti za kumpinga Trump. Wengine walionekana nje ya Ikulu ya Marekani wakipaza sauti kuwa “Not my president” (Si Rais wangu), pamoja na mabango mengine.


Wengi wa waandamanaji walioongea na CNN wameelezea kuwa wana wasiwasi sana kuhusu Trump kwa vile kuongoza Marekani sio kama kuiongoza nchi yoyote duniani.


“Kwa matokeo haya tumeiangusha Dunia. Trump hakustahili kuwa Rais. Nahisi watu walipiga kura kwa hasira lakini Trump ni hatari kwa dunia,” alisema mmoja wa waandamanaji aliyejitambulisha kwa jina la James Betwell kutoka Califonia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post