RAIS MAGUFULI KUFANYA MAHOJIANO NA WAANDISHI WA HABARI LEO DAR


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 04 Novemba, 2016 atafanya mahojiano ya kwanza na waandishi wa habari tangu aingie madarakani mwaka mmoja uliopita.

Mahojiano haya yatarushwa moja kwa moja na vituo vya habari vya redio na televisheni kutoka ukumbi wa Ikulu Jijini Dar es Salaam na yataanza saa 4:00 asubuhi.

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais inapenda kuwaalika wananchi wote kusikiliza na kutazama mahojiano hayo ili mpate fursa ya kujua mambo mbalimbali ambayo Mheshimiwa Rais atayatolea majibu.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post