POSTA YATANGAZA KUFUKUZA WAFANYAKAZI WOTE WABADHIRIFU WA SHILINGI BILIONI 13


Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta, Dk Haruni Kondo


BODI ya Wakurugenzi na Menejimenti ya Shirika la Posta Tanzania imetangaza kufukuza wafanyakazi wote wa shirika hilo waliojihusisha na ubadhirifu wa Sh bilioni 13 kupitia wizi wa mafuta ya magari ambayo yamekuwa yakilipwa kwa magari ambayo ni mabovu.

Hatua hiyo imekuja baada ya bodi hiyo kufanya ziara Dar es Salaam kwenye maeneo yaliyoonesha kuwa mikataba yake ina mashaka, ili kujiridhisha na kuchukua hatua.

Mwenyekiti wa bodi hiyo, Dk Haruni Kondo, alisema wamebaini ubadhirifu uliofanywa kwa magari mabovu ambayo yapo gereji, lakini yamekuwa yakipewa mafuta kwa miezi 18 ambapo gharama ya mafuta hayo imefika Sh bilioni 13 mpaka sasa. Alisisitiza watumishi wachache wanaofanya vitendo vya namna hiyo wataondolewa ili kuleta ufanisi katika shirika hilo.

“Unakuta magari yameharibika yapo gereji lakini yananyonya mafuta. Watu kama hao hawatakiwi ni kuwaondoa tu,” alisema.

Aliongeza kuwa ubadhirifu mwingine waliougundua ni ule ambao unafanywa na madereva wa magari ya mizigo ambayo yanakuwa yamesheheni mizigo ya Sh milioni 10, lakini inapofikishwa sehemu husika wahusika wanadai mizigo hiyo ni ya Sh 500,000.

Dk Kondo alisema suala hilo limekuwa ni tatizo kwenye mali za shirika hilo, kwani hata pale bodi inapotaka taarifa kwa 

ajili ya kujiridhisha inapata usumbufu.

Chanzo-Habarileo




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527