Picha 20: WAANDISHI WA HABARI SHINYANGA WAPEWA ELIMU YA KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO


Jumatano,Novemba 09,2016- Hapa ni katika ofisi ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club- SPC) ambapo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wilaya ya Shinyanga limekutana na waandishi wa habari na kuwapatia elimu kuhusu namna ya kukabiliana na majanga ya moto. 

Elimu hiyo imetolewa na Afisa Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wilaya ya Shinyanga,Mkaguzi Msaidizi Benjamin Kinenge aliyekuwa ameambatana na Afisa Habari wa jeshi hilo wilaya ya Shinyanga Felix Banzi. 

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo,Kinenge alisema miongoni mwa majukumu ya jeshi hilo ni kuzima moto ili kuokoa maisha na mali za raia na kuhakikisha hakuna madhara yanayoweza kujitokeza. 

“Ili kutekeleza majukumu yetu tunahitaji ushirikiano wa wadau mbalimbali wakiwemo wananchi ndiyo maana tunaendelea kutoa elimu katika makundi mbalimbali kuhusu namna ya kukabiliana na majanga ya moto”,alisema Kinenge. 

Aliwataka wananchi kutoa taarifa kwa jeshi hilo pindi panapotekea tukio lolote la dharura kama vile ajali za vyombo vya usafiri,moto katika majengo,kutumbukia chooni,kisimani,kwenye bwawa,kufukiwa na kifusi na matukio mengine. 

“Kama kuna tukio toa taarifa mapema kwa jeshi la uokoaji mkoa wa Shinyanga kupitia namba zifuatazo Bure (Vodacom na Tigo) namba 114,zingine ni TTCL 028 2762600,Tigo 0679542351 na Vodacom 0752565490,pigeni simu katika namba hizi mapema ili tuwahi eneo la tukio ili tuweze kuzima moto na kufanya uokoaji kwa haraka zaidi”,alifafanua. 

Kwa upande wake katibu wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga Stephen Wang’anyi alilishukuru jeshi hilo kwa kuona umuhimu wa kukutana na waandishi wa habari na kuwapa elimu kuhusu namna ya kukabiliana na majanga ya moto majumbani na katika ofisi. 

Hata hivyo alitumia fursa hiyo kuliomba jeshi hilo kufikisha elimu kwa wananchi wengi zaidi sambamba na kusambaza namba za mawasiliano zinazotumika wakati wa matukio ya dharura ili wananchi waweze kutoa taarifa kwa jeshi hilo wakati yanapojitokeza matukio. 

Angalia picha hapa chini matukio yaliyojiri wakati wa mafunzo hayo 
Hapa ni ndani ya ofisi ya klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga SPC- ,Kushoto ni mwenyekiti wa SPC,Kadama Malunde,katikati ni Afisa Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wilaya ya Shinyanga,Mkaguzi Msaidizi Benjamin Kinenge ,kulia ni Afisa Habari wa jeshi hilo wilaya ya Shinyanga Felix Banzi .Picha zote na Suleiman Abeid- Malunde1 blog
Waandishi wa habari wakiwa ofisini na maafisa kutoka jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Shinyanga
Kulia ni Afisa Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wilaya ya Shinyanga,Mkaguzi Msaidizi Benjamin Kinenge akitoa elimu kwa waandishi wa habari kuhusu namna ya kukabiliana na majanga ya moto.Kushoto ni mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga,Kadama Malunde
Waandishi wa habari wakiandika dondoo muhimu
Mafunzo yanaendelea
Afisa Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wilaya ya Shinyanga,Mkaguzi Msaidizi Benjamin Kinenge akielezea somo la moto/sayansi ya moto
Mafunzo yanaendelea
Afisa Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wilaya ya Shinyanga,Mkaguzi Msaidizi Benjamin Kinenge akionesha kimiminika kinachotumika kuzimamoto
Afisa Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wilaya ya Shinyanga,Mkaguzi Msaidizi Benjamin Kinenge akifundisha kwa vitendo somo la moto na namna ya kuzima moto Fire Extinguisher
Afisa Habari wa jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Shinyanga Felix Banzi akionesha kwa vitendo namna ya kuzima moto kwa kutumia Fire Extinguisher
Waandishi wa habari wakiangalia moto
Moto unawaka
Mwandishi wa habari kutoka Radio Faraja,Jenifer Paul Mahesa akizima moto kwa kutumia Fire Extinguisher
Waandishi wa habari wakiendelea kupata elimu  kutoka kwa maafisa wa jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Shinyanga
Katibu wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga Stephen Wang’anyi akizima moto
Katibu wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga Stephen Wang’anyi akiendelea kuzima moto
Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga,Kadama Malunde akizima moto
Afisa Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wilaya ya Shinyanga,Mkaguzi Msaidizi Benjamin Kinenge akiendelea kutoa elimu ya sayansi ya moto
Waandishi wa habari wakifuatilia somo
Afisa Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wilaya ya Shinyanga,Mkaguzi Msaidizi Benjamin Kinenge akielezea umuhimu wa kuwa na vifaa vya kuzimia moto majumbani na ofisini.
Picha zote na Suleiman Abeid- Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post