Maombolezo Kwa Watu 80 Yafanyika Afghanistan


Raia kote nchini Afghanistan wanashiriki katika siku ya maombolezo, kufuatia shambulio la bomu la mlipuaji wa kujitoa mhanga, lililofanyika jana Jumamosi katika mji mkuu wa nchi hiyo-Kabul.

Watu themanini waliuwawa, huku zaidi ya 200 walijeruhiwa.

Mlipuaji bomu alikuwa akiwalenga waandamanaji wa jamii ndogo ya Hazara - ambao wengi wao ni waislamu wa Ki-Shia.

Kundi la Islamic State - linachoshirikisha wapiganaji wenye msimamo mkali wa waisalmu wa Ki-Sunni- kimekiri kuhusika na shambulio hilo.

Rais wa Afghan, Ashraf Ghani, ameahidi kulipiza kisasi.

Ujumbe wa Umoja wa mataifa nchini Afghanistan, umetaja shambulio hilo kama uhalifu wa kivita.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post