Jamaa Avamiwa na Nyoka Chumbani Kwake Akiwa Amelala
Wednesday, June 22, 2016
Nyoka mkubwa ambaye alikuwa akiishi katika dari ya nyumba moja nchini Australia kwa takriban miaka 10 sasa ameamua kuingia katika chumba cha kulala.
Mwenye nyumba hiyo Trina Hibberd kutoka eneo la Queenland aliamka siku ya Jumatatu na kumuona nyoka huyo mwenye urefu wa mita 5.2 amejipinda katika kitanda chake.
Aliwasha taa ya chumba hicho kabla ya mtaalam wa kushika nyoka Dave Goodwin kuwasili.
Bw Goodwin aliamua kumdunga sindano ya kulala nyoka huyo mwenye kilo 40 kabla ya kumuweka katika mkono wake na kuondoka naye.
Via>>BBC
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com
Social Plugin