RAIS SHEIN "UPINZANI HAUJAKIDHI VIGEZO VYA KUTOA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS"



Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein amesema hakuna chama kilichokidhi matakwa ya kikatiba kutoa makamu wa kwanza wa Rais.


Rais Shein aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na Baraza la Wawakilishi visiwani Zanzibar kwa mara ya kwanza tangu kuchaguliwa kwake kwa mara ya pili kuongoza Umma wa Wazanzibar.


''Hakuna Chama chama kinachokidhi kutoa makamu wa kwanza wa Rais huo ni uamuzi wa wananchi na ni uamuzi wa kidemokrasia unaostahili kuheshimiwa ''Alisema Rais Shein.


Aidha Rais Shein katika hotuba yake kwa Baraza hipo pamoja na wananchi wa Zanzibar aliahidi kuhakikisha Zanzibar inasonga mbele kimaendeleo kwa kujenga viwanda maeneo mbalimbali na kuboresha huduma za kijamii pamoja na kupandisha mishahara hadi kufikia shilingi laki 3 kwa kima cha chini.


Pia Rais Shein alisema ataongoza Zanzibar kwa haki na watu wote ni lazima wafahamu kwamba yeye ndiye Rais ambaye alichaguliwa kwa asilimia 91.4 hivyo uchaguzi haupo tena hadi mwaka 2020.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post