MFUKO WA HABARI TANZANIA TMF WASEMA UKO TAYARI KUGHARAMIA MATANGAZO YA LIVE BUNGENI

 
Mkurugenzi Mtendaji wa mfuko wa Habari Tanzania (TMF) Ernest Sungura amesema taasisi yake iko tayari kugharamia matangazo ya live Bungeni kupitia TBC ili kuwawezesha wananchi kujua kinachoendelea Bungeni.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika mkutano na wahariri na wamiliki wa vyombo vya habari nchini mbele ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari( MAELEZO), Assah Mwambene, Sungura amesema lengo la TMF ni kuleta mabadiliko chanya katika tasnia ya habari na kuona wananchi wanapata taarifa kwa wakati.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527