MAGUFULI AAGIZA PESA ZA SHEREHE YA WABUNGE ZIKASAIDIE MUHIMBILI,ZIKO HAPA SENTENSI ZAKE ZA HATARI





Rais John Pombe Magufuli ameagiza kuwa fedha zilizochangwa kwa ajili ya sherehe iliyokuwa imeandaliwa kwa ajili ya wabunge na yeye kualikwa, zipelekwe katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Magufuli ametoa agizo hilo baada ya kuhudhuria sherehe hiyo na kupokea taarifa kuwa kiasi cha shilingi milioni 225 kilikuwa kimechangwa na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za kibenki kwa ajili ya sherehe hiyo ya uzinduzi wa bunge


Kwa mujibu wa Afisa wa Bunge Bw. Said Yakubu, Rais Magufuli ameagiza katika sherehe hiyo zitumike shilingi milioni 24 pekee na nyingine ziende Muhimbili zikasaidie kununua vitanda ili kupunguza tatizo la wagonjwa kulala chini.

Yakubu amesema kuwa agizo hilo la Rais limetekelezwa.



Ziko hapa Sentensi kadhaa za Rais John Pombe Magufuli akiwa Bungeni Dodoma


Rais @MagufuliJP : Yote tuliyowaahidi tutayafanya kwelikweli, sikuahidi ili nipigiwe kura bali ili kuyatimiza yote

Rais @MagufuliJP : Siku ya Tarehe 25 Oktoba ilikuwa ni ya furaha sana, kuna watu walifikiri tutafarakana lakini wameshangaa

Rais @MagufuliJP : Nampongeza @zittokabwe kwa kuonesha utulivu, yeye hakupiga kelele, nahitaji Tanzania ya aina hii

Rais @MagufuliJP :Kati ya maeneo mengi yaliyolalamikiwa kwenye kampeni ni RUSHWA,lingine ni upotevu wa fedha za halmashauri

Rais @MagufuliJP : Eneo lingine ni tatizo la maji, na lingine ni TRA kushindwa kukusanya kodi na kuachia ukwepaji kodi

Rais @MagufuliJP : Eneo lingine ni migogoro ya ardhi, TANESCO, huduma za afya na Maliasili

Rais @MagufuliJP : Haiwezekani meno ya tembo yakamatwe nchi za watu huko bila watu wa idara husika kuhusika

Rais @MagufuliJP : Suala lingine ni kuhusu elimu, viwanda n.k Ni lazima niyaseme haya ili tujue wapi tunaanzia

Rais @MagufuliJP : Mimi ni muumini wa muungano, niliapa kuulinda muungano, hata nisipoapa, ni lazima niulinde muungano

Rais @MagufuliJP : Suala lingine ni kuimarisha miimili ya serikali, serikali itahakikisha miimili yote inaimrika.

Rais @MagufuliJP : Kwa upande wa bunge tutahakikisha fedha za mfuko wa bunge zinapatikana kwa wakati

Rais @MagufuliJP : Kuhusu Katiba, nimepokea kiporo kutoka kwa serikali ya awamu ya 4, tutarekebisha sheria katiba ipatikane

Rais @MagufuliJP : Kuhusu uchumi, tutaimarisha miundombinu iliyopo na kujenga mipya ili kuvutia wawekezaji

Rais @MagufuliJP : Kuhusu viwanda, serikali ya awamu ya tano itaweka uzito mkubwa katika viwanda. Natambua wawekezaji

Rais @MagufuliJP :Tutaanza na viwanda vilivyopo na kuhakikisha vinafanya kazi, waliokuwa hawaviendelezi niliwataka kuviacha

Rais @MagufuliJP :Hatuwezi kuwa na watu wanajiita wawekezaji, tunawapa viwanda vyetu halafu wanaviatamia tu kama mayai

Rais @MagufuliJP : Kuna wengine wameamua hata kufugia mbuzi majengo ya viwanda vyetu

Rais @MagufuliJP : Watendaji wa serikali watakaosababisha vikwazo kwa wawekezaji hatutakuwa na nafasi zao

Rais @MagufuliJP : Sura ya tatu ya viwanda ni kuzalisha ajira nyingi, nataka sekta ya viwanda ichangie 40% ya ajira zote

Rais @MagufuliJP : Tutazingalia sekta za mifugo, kilimo na uvuvi kwa jicho la kibishara, watanzania wengi wanazitegemea

Rais @MagufuliJP : Makodi yote ya ovyo ovyo ambayo ni kero kwa wakulima wetu tutayaondoa kama si kuyapunguza yote

Rais @MagufuliJP : 28.2% ni masikini, lazima tushughulikie umasikini kwa kupunguza tofauti kati ya walionacho na wasionacho

Rais @MagufuliJP : Hatuwezi kuendeleza viwanda ikiwa hatujawekeza kwa vijana kwa kuwapa ujuzi na maarifa

Rais @MagufuliJP : Tutahakikisha shule na vyuo vyetu vinaandaa vijana wenye uwezo, ujuzi na maarifa na watapatiwa mikopo.

Rais @MagufuliJP : Tutawawezesha vijana kujitafutia maisha yao kama vile bodaboda, mama lishe, machinga n.k

Rais @MagufuliJP : Kodi ambayo haikusanywi ni nyingi na ingeweza kuendesha nchi, lakini tunahangaika na watanzania wanyonge

Rais @MagufuliJP :Kila kijiji kitakuwa na zahanati, kila kata kitakuwa na kituo cha afya na kila wilaya hospitali ya wilaya

Rais @MagufuliJP :Tutaboresha huduma za afya maana imekuwa ni mazoea mtu akiugua hata mafua anaenda kutibiwa nje ya nchi

Rais @MagufuliJP : Kuanzia Januari mwakani wanafunzi watasoma bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne.

Rais @MagufuliJP : Dawa za kulevya. Tutakabiliana na mtandao mkubwa wa madawa ya kulevya, tutatafuta wale wahusika wakubwa

Rais @MagufuliJP : Nachukizwa sana na vitendo vya rushwa na ufisadi, vitendo hivi vinawatia hasara kubwa sana watanzania

Rais @MagufuliJP : Chama changu cha @ccm_tanzania kimejengwa katika misingi ya kuchukia rushwa na ufisadi,

Rais @MagufuliJP : Sina uhakika kama sasa ndani ya CCM hakuna watu wanaotoa na kupokea rushwa

Rais @MagufuliJP : Dawa ya jipu ni kulitumbua, na mimi nimejipa kazi ya kuwa MTUMBUA MAJIPU, naomba wabunge mniunge mkono

Rais @MagufuliJP : Ili kusimamia kazi ya kutumbua majipu nimesema nitaanzisha mahakama ya rusha na mafisadi

Rais @MagufuliJP : Kama nimeteua mtu yoyote halafu nikabaini kuwa anahusika na vitendo vya rushwa na ufisadi NITAMTIMUA

Rais @MagufuliJP : Watendaji wazembe hawatavumiliwa katika serikali yangu, tumewavumia vya kutosha, wakati sasa umekwisha

Rais @MagufuliJP : Tutahakikiksha kila mtu anayestahili kulipa kodi, analipa kodi, unaponunua bidhaa yoyote dai risiti

Rais @MagufuliJP : Tutahakikisha safari zote za nje ya nchi zinadhibitiwa ili kuongeza mapato

Rais @MagufuliJP : Katika mwaka 2013/14 zaidi ya bilion 300 zilitumika kwa safari za nje na zingeweza kuwatumikia wananchi

Rais @MagufuliJP : Idara zilizoongoza kwa safari za nje ni Bunge, mambo ya nje, Wizara ya Fedha, Wizara ya mambo ya ndani

Rais @MagufuliJP :Pia tunazuia ziara za mafunzo nje ya nchi, huyo mnayeenda awafundishe kwanini msimuite aje hapa kwetu

Rais @MagufuliJP : Kuna watu hapa wameshasafiri nje ya nchi mara nyingi zaidi kuliko walivyosafiri kwenda kwa wazazi wao

Rais @MagufuliJP : Sheria ya manunuzini mbaya, unaweza kukuta kalamu ya Bic inayouzwa Tsh. 1000 inanunuliwa kwa Tsh. 10,000

Rais @MagufuliJP : Bunge ni chombo muhimu, halipaswi kuwa chombo la mipasho, kutukanana, kutoka nje, n.k

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post