ETHIOPIA WAMEANZA KUTUMIA TRENI ZA ABIRIA ZINAZOTUMIA UMEME,ANGALIA PICHA NA VIDEO HAPA



Nimepita kwenye page ya Facebook ya BBC Swahili nikakutana na hii stori ambayo nimeguswa kuishare hata hapa Malunde1 blog kuhusu nchi ya Ethiopia kuzindua Treni za umeme.





Ripoti inasema Treni hizi ambazo zimezinduliwa September 20 2015 zinaanza kubeba abiria na zinatarajiwa kurahisisha usafirishaji wa watu kwenye mji mkuu wa Addis Ababa,Ethiopia nchi ambayo mpaka mwaka huu wanasema idadi ya watu wake ni zaidi yaMILIONI 90.


BBC wanasema hizi Treni zimetajwa kuwa mfano na za kwanza kusini mwa jangwa la sahara ambapo ujenzi na uendeshaji wa huduma hii ya reli unatekelezwa kwa ushirikiano na serikali ya China.



Picha zote ni kutoka BBC.

Treni hizi za umeme zitakua na uwezo wa kuhudumia Abiria elfu kumi na tano ndani ya dakika 60 ambapo Treni moja inaweza kubeba abiria 286 kwa wakati mmoja.

TAZAMA VIDEO YA TRENI ZA ETHIOPIA ZILIVYOFANYIWA MAJARIBIO MARA YA KWANZA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post