CCM Noma!! WEMA SEPETU APIGWA CHINI UBUNGE VITI MAALUM


Msanii wa Filamu za kibongo anayeongoza kwa urembo ndani ya tasnia hiyo, Wema Abraham Sepetu, aliyekuwa anagombea Ubunge wa Viti Maalum jimbo la Singida amebwagwa chini baada ya kupata kura 90 tu katika uchaguzi huo.


Mgawanyo wa kura ulikuwa hivi;
1. Aysharose Mattembe (311)
2. Martha Mlata(235)
3. Diana Chilolo(182)
4. Wema Sepetu(90)

Baada ya matokeo hayo, Lulu Michael amemtia moyo Wema Sepetu kwa Kuandika ujumbe huu;

Kuna matokeo ya aina 3
>>Kushinda
>>Kushindwa
>>Kudroo.

Mpaka hapa ulipofika Leo umethubutu kitu ambacho wanawake wengi ni waoga kujaribu wewe ni mshindi Dada yawezekana Kuna kingine zaidi Mungu amekuandalia

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527