WAENDESHA BODABODA SHINYANGA MJINI WAPIGWA MABOMU NA POLISI WAKIANDAMANA NA KUFUNGA BARABARA

Askari polisi wa FFU wakiwadhibiti waendesha bodaboda mjini Shinyanga-Picha  zote na Marco Maduhu-Malunde1 blog



Waendesha bodaboda wakiwa barabarani
Askari polisi wakiwa barabarani kuzuia waendesha bodaboda wasizuie magari
Waendesha bodaboda wakiwa wamefunga barabara

Askari polisi wakiwa eneo la tukio-picha zote na Marco Maduhu-Malunde1 blog



Katika hali isiyokuwa ya kawaida jeshi la polisi mkoani Shinyanga limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda baada ya kuandamana kwenda kwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga kasha  kufunga barabara kuu ya kutoka Mwanza kuelekea Tabora wakidai wamechoka kuonewa na jeshi hilo.

Vurugu hizo zimetokea leo saa tano asubuhi ambapo waendesha pikipiki  hao waliandamana kwenda kwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga, ili kuwasilisha kero zao za jeshi la polisi, ambapo wamekuwa wakiwaonea bila ya kufuata sheria, na kuwafanya kuwa kama vitega uchumi vyao.


Kutokana na hali hiyo askari wa jeshi la polisi walitanda katika ofisi za mkuu wa mkoa wa Shinyanga kukabiliana na bodaboda hao ambao baada ya zoezi la kumuona mkuu wa mkoa kushindikana waliamua  kufunga barabara kuu itokayo Mwanza kuelekea Tabora.

Kufuatia kitendo cha   kuzuia mabasi kwa muda hali hiyo iliyolazimu jeshi la polisi kuingilia kati na kuwatawanya na
ndipo walipochukua sheria mkononi na kuanza kuwarushia mawe askari hao kitendo kilichosababisha kuanza kurusha mabomu na kuanza kuwapiga na virungu.

Waendesha bodaboda hao amesema ,askari hao hasa wanaotembea na pikipiki barabarani maarufu kama (Makhirikhiri),wamekuwa wakiwanyanyasa kwa kuwakamata hovyo, huku wakiwavizia kwenye kona na kwamba licha ya kuviziwa kwenye kona wamekuwa wakiwavamia vijiweni huku wakiwa wamepaki pikipiki na kuzifunga minyororo, kuwatoza stika za wiki ya usalama barabara ambazo muda wake umeshapita.

Wamedai kuwa askari haowamekuwa wakiwakimbiza na kuwachapa fimbo migongoni, pamoja na kuwaomba rushwa mara wanapo wakamata licha ya kuwakuta hawana makosa.

Kamanda wa Jeshi la polisi mkoani Shinyanga Justus Kamugisha akizungumza na waandishi wa habari eneo la tukio, amethibitisha kukamata waendesha bodaboda tisa, na watafikishwa mahakamani kwa kosa la kuchochea vurugu na kuandamana bila kibali.

Na Marco Maduhu-Malunde1 blog 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post