Hii Inatoka Shinyanga!! MKE WA AFISA MIFUGO AJINYONGA KWA KATANI KWENYE BANDA LA KUKU!!

Matukio ya watu kujinyonga yameendelea kujitokeza mkoani Shinyanga ambapo ,mwanamke aitwaye Sarah Lucas(25) mkazi wa kijiji cha Negezi kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu mkoani Shinyanga ,amekutwa amefariki kwa kujinyonga kwa kutumia kamba ya katani kwenye banda la kuku.

Kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga amesema tukio hilo limetokea Machi 29 mwaka huu majira ya saa tisa alasiri ambapo mwanamke huyo ambaye ni mke wa afisa mifugo wilayani Kishapu alikutwa amejinyonga  kwa kutumia kamba ya katani nyumbani kwake kwenye banda la kuku.

Ameongeza kuwa baada ya majirani zake kubaini kuwa mwanamke huyo kuwa amefariki ,ndipo walipotoa taarifa kwa jeshi la polisi ambalo lilifika eneo la tukio na kuukuta mwili huo ukiwa kwenye banda la kuku nyumbani kwake.
 
Amesema katika uchunguzi wa awali walikuta marehemu ameacha ujumbe wa maandishi unaosema kuwa "nashukuru mume wangu tumeishi wote, naomba umtunze mwanangu na kumsomesha na upo tayari kuoa mwanamke mwingine".
Na Kadama Malunde-Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527