Mara ya kwanza mwanamke huyu alipatwa na
tukio kama hili miaka kumi iliyopita, alipoenda kuripoti tukio hilo
Polisi mtuhumiwa wa kosa la kumuingilia kwa nguvu mwanamke huyu
ilishindikana kukamatwa kutokana na kukosekana kwa ushahidi.
Safari hii mwanamke huyo Adele Barber ameamua kumng’ata ulimi mwanaume ambaye amembaka ili kupeleka polisi upatikane ushahidi wa DNA.
Akisimulia tukio hilo amesema alikuwa
anapita kwenye uchochoro huko Dunstable, England akasikia mtu anakuja
nyuma yake lakini hakuhisi chochote, jamaa huyo alimkimbilia kwa nyuma
na kumsukuma kwenye uzio, wakati anataka kumbaka alimng’ata ulimi,
kuukata na kubaki na kipisi mdomoni na kwenda nacho nyumbani, mume wake
akawaita Polisi na kuwapa ushahidi huo ambao ulisaidia mtuhumiwa
kukamatwa.