KUHUSU TAARIFA ZA KIFO NA MAZISHI YA PADRE JOSEPH MAYUNGA WA JIMBO KATOLIKI LA SHINYANGA


Padre Joseph Mabula Mayunga enzi za uhai wake akipatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya Bugando jijini Mwanza
Mwili wa Padre Joseph Mabula Mayunga  aliyefariki dunia January 17 mwaka huu  katika hospitali ya rufaa ya Bugando jijini Mwanza leo umewasili katika Parokia ya Mwadui ambayo aliihudumia kwa muda mrefu enzi za uhai wake.

Mwili huo umewasili katika parokia hiyo  ili kutoa nafasi kwa waamini wa parokia hiyo kutoa heshima zao za mwisho.

Waumini hao wa parokia ya Mwadui pia wameshiriki misa takatifu ya kumwombea marehemu ambayo imeongozwa na paroko wa parokia ya Sayusayu na Gambela wa seminari ya Awali ya Sayusayu padre Martin Mihango.

Kesho Alhamis mwili wa marehemu Padre Mayunga utapelekwa parokia ya Buhangija mjini Shinyanga  ambapo pia amewahi kufanya kazi enzi za uhai wake ili kutoa fursa kwa waamini wa parokia hiyo kutoa heshima zao za mwisho na baadaye kushiriki misa maalumu ya kumwombea.

Padre Mayunga ambaye amefanya kazi katika parokia mbalimbali za jimbo la Shinyanga ikiwemo parokia ya Mwadui na Buhangija,amefariki dunia katika hospitali ya rufaa ya Bugando alikokuwa akitibiwa kutokana na kuugua maradhi ya shinikizo la damu na kisukari.

Mazishi ya Padre Mayunga  yanatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa terehe 23,2015 katika makaburi ya mapadri yaliyopo katika Kanisa kuu la Mama Mwenye Huruma la Ngokolo mjini Shinyanga.

Mazishi hayo yatatanguliwa na misa ya kumwombea itakayoongozwa na askofu mkuu wa jimbo kuu la Mwanza na msimamizi wa kitume wa jimbo katoliki la Shinyanga mhashamu Yuda Thadeus Ruwaich.
Uongozi wa Malunde1 blog unawapa pole ndugu,jamaa na marafiki wote waliofikwa na msiba huo.
Mungu aiweke mahali pema mbinguni roho ya marehemu Padre Joseph Mabula Mayunga. amen!
Na Simeo Makoba-Shinyanga


Bonyeza hapa Tukupe habari zote mara tu Tunapozitoa "HABARI" VITUKO "MAPENZI"MAGAZETI,UDAKU>
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba  +255 688 405 951

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post