WATU 69 WAFARIKI,WENGINE 196 HOI BAADA YA KUBUGIA POMBE YA KIENYEJI YENYE SUMU

Zaidi ya Watu 69 wamepoteza maisha Msumbiji  baada ya kunywa  pombe ya kienyeji  inayosadikiwa  kuwa na sumu walipokuwa wakihudhuria mazishi na wengine 46 kulazwa Hospitali.

Afisa afya  nchini humo Alex Albertini, amesema wanaamini kuwa kilevi hicho cha kienyeji kilichotengenezwa kwa mtama na mahindi kilikuwa na sumu na kuna hatari ya vifo  kuongezeka kutokana na kukosekana kwa vifaa  huku watu 196 wakiripoti Hospitali kupatiwa matibabu.
Uchunguzi wa Polisi umegundua kwamba pombe hiyo ilikuwa imewekwa  sumu ya nyongo ya mamba na kusema wale waliokunywa wakati wa asubuhi  hawakuwa na dalili zozote wakati wale waliokunywa  mchana waliugua na wengine kufariki.
Mwanamke aliyetengeneza pombe hiyo pamoja na ndugu zake nao walifariki.
Sample ya damu za watu waliofariki imepelekwa Maputo kwa ajili ya vipimo huku Serikali ikitangaza maombolezo ya siku tatu kutokana na tukio hilo.
1 (1)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post