Zaidi ya watu 40 wamenusurika
kifo huku mmoja akikatika viungo vya miguu na wengine kujeruhika vibaya
baada ya lori moja lilionekana kuwa ni la jeshi kugongana uso kwa uso
na gari la abiria aina ya COSTA la Ubungo -Tegeta eneo la Tegeta jijini Dar es salaam.
Tukio hilo limevuta hisia za mamia ya wakazi wa
Tegeta huku baadhi ya mafundi gereji wa Tegeta wakijaribu kutumia vifaa
maalumu kukata mabati ya magari kwa nia ya kunasua baadhi ya majeruhi
walionasa ndani ya COASTA hiyo kusuru abiria walioonekana kunasa katika
vyuma vya magari hayo.
Baadhi ya mashuhuda na dereva wa COSTA pamoja na
kuomba eneo la kibaoni kuweka njia ya mzunguko maarufu kama ROUND ABOUT
kwa lengo la kuepusha madereva wanao lazimika kugeuza kwa dharura
katika njia kuu maarufu kama UTAN kutokana na njia hiyo kukosa fursa ya
kugeuza endapo kuna ulazima wa kufanya hivyo.
Pia wamemtupia lawama Dereva wa Lori kama msababisha ajali kwa kukosa hekima ya kuchukua
tahadhari kabla ya kufanya hivyo.
Kamanda wa polisi mkoa kipolisi Kinondoni Kamilius Wambura amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo akieleza kutoa taarifa mara baada ya uchunguzi kufanyika.