Utata umeibuka baada ya sister wa Kanisa Katoliki huko Italy aliyekuwa akilalamikia maumivu ya tumbo na kukimbizwa Hospitali na
kujifungua mtoto wa kiume licha ya kuishi katika Jumuiya hiyo ya
wanawake pekee
Sister huyo mwenye umri wa miaka 31 yupo kwenye kikundi cha masista cha Santa Chiara Italy,
asili yake ni Amerika ya Kusini, alilalamikia maumivu makali ya tumbo
baadaye alianguka, madaktari walifika katika eneo hilo na baada ya
kumfikisha Labour alijifungua.
Watu wengi wameshindwa kuelewa kwa jinsi gani ameweza kupata ujauzito licha ya kula kiapo cha usafi wa moyo na utii.
Tukio
linalofanana na hili lilitokea mwaka jana baada ya sister mmoja wa
Salvador ambaye umri wake ni miaka 33 ambaye alijifungua mtoto wa kiume
na kumpa jina la Papa Francis.