Binti
mmoja mwenye umri wa miaka 19, Rukia Ally anadaiwa kumuua kwa kumchoma
kisu kaka yake wa kuzaliwa, Said Ally wote wakazi wa Tegeta Mivumoni
jijini Dar es Salaam, kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kutokana na kijana
huyo kutaka kudhibiti tabia zisizofaa za dada yake huyo ikiwemo umalaya, tukio
lililotokea usiku wa Januari 24 mwaka huu.
Inadaiwa kuwa siku hiyo,
msichana huyo hakuwa amerudi nyumbani kwa siku tatu, hivyo aliporejea
saa tatu usiku, kaka yake alimuuliza alikokuwa lakini alishindwa kutoa
majibu ya kueleweka, kaka huyo alimchapa na fimbo mguuni kama ishara ya
kumkanya, lakini inadaiwa Rukia alichomoa kisu alichokuwa amekificha
nguoni mwake na kumchoma nacho upande wa kushoto wa kifua chake.
Chanzo-Kibonajoro.com
Chanzo-Kibonajoro.com