NB-Picha haihusiani na habari hapa chini |
Watu watano wamefariki dunia akiwemo dereva wake baada ya gari
waliyokuwa wamepanda aina ya Noah kupasuka tairi la nyuma na kuacha
njia hivyo kusababisha vifo vya watu hao katika eneo la Fukayosi katika
Tarafa ya msata wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei
alisema kuwa ajali hiyo ilihusisha gari namba T 252 DCB aina ya Toyota
Noah lililokuwa likiendeshwa na Ramadhana Masapala (32) lilikuwa
likitokea kwenye kituo cha afya cha Miono kuelekea hospitali ya wilaya
ya Bagamoyo.
Kamanda Matei alisema kuwa ndani ya gari hiyo alikuwepo mama
mjamzito aliyekuwa akipelekwa hospitali Shukuru Jaba (30) na muuguzi wa
kituo cha afya cha Miono Mariamu Omary ambao wao walijeruhiwa.
Alisema wote waliofariki dunia walikuwa ni wakazi na wakulima wa
Miono na kuwa miili ya marehemu hao imepelekwa hospitali ya Wilaya ya
Bagamoyo huku majeruhi wawili wakipelekwa kituo cha afya cha Miono huku
mama mjamzito akiandaliwa kupelekwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa
matibabu zaidi.
Via>>ITV
Bonyeza hapa Tukupe habari zote mara moja zikitoka
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba +255 688 405 951