AFISA WA SUMATRA ANUSA KIPIGO KUTOKA KWA ABIRIA

Afisa mmoja wa mamlaka ya usafirishaji  nchi kavu na majini (SUMATRA) mkoani kilimanjaro  amenusurika kipigo kutoka kwa abiria baada ya kuchana kibali cha mabadiliko ya ratiba ya bus la Ibra Line walilokuwa wakisafiria toka moshi kwenda dar badala ya arusha kwenda Dar na kulizuia  lisiendelee  na safari  kwa madai ya kukiuka ratiba.


Vurumai hiyo ilitokea katika eneo la njiapanda baada ya afisa huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana kuchana kibali cha mabadiliko ya ratiba ya bus hilo bus hilo  la kampuni ya ibra line lenye namba za usajili t 288 CDV na abiria hao kuja juu wakitaka waendelee na safari.
 
Abiria hao wamesema, sumatra hawakuwa na sababu za msingi za kuchana kibali hicho ambacho kimetolewa na afisa wa usalama barabarani mkoani k'njaro kwa dharura na kuwachelewesha safari yao kwa kuondoka saa sita mchana badala ya saa mbili asubuhi.
 
Mkurugenzi wa kampuni hiyo  bw ibrahimu shayo amesema, BUS hilo liliharibika  wakati likiwa njiani kwenda arusha  na kufanyiwa matengenezo mjini moshi na asubuhi yake lililazimika kuanzia safari yake moshi badala ya arusha baada ya kupata kibali hicho kutoka kwa mkaguzi wa usalama barabarani mkoani kilimanjaro.
 
Afisa wa sumatra mkoani kilimanjaro bw tadey mwita amesema,bus hilo lilizuiliwa njiapanda ili kupata ushahidi wa ukiukwaji wa ratiba na kuliruhusu bus hilo liendelee  na abiria wake saa sita kasorobo mchana katika eneo la makao makuu ya sumatra mjini moshi wakati suala hilo likifanyiwa kazi kwa mujibu wa sheria.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post